Pata taarifa kuu
HAKI-SIASA

DRC: Salomon Idi Kalonda, mshauri maalum wa Moïse Katumbi akamatwa

Hali ya kisiasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inazidi kuwa ngumu miezi sita kabla ya uchaguzi mkuu. Mnamo Mei 30, 2023, katika mji mkuu Kinshasa, mwanasiasa wa upinzani Salomon Idi Kalonda, mshauri maalum wa Moïse Katumbi, aliyetangazwa kuwa mgombea wa uchaguzi ujao wa urais, amekamatwa na idara za ujasusi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa N'djili alipokuwa akijiandaa kuondoka Kinshasa na kiongozi wake.

Salomon Idi Kalonda, mshauri maalum wa Moïse Katumbi azuiliwa na idara za za usalama.
Salomon Idi Kalonda, mshauri maalum wa Moïse Katumbi azuiliwa na idara za za usalama. AFP/File
Matangazo ya kibiashara

Upinzani na mashirika ya kiraia yamelaani kitendo hicho huku Moïse Katumbi anazungumzia kitendo hicho kuwa ni utekaji nyara "mbaya"; ni demokrasia ambayo 'imeangamizwa', anasema Waziri Mkuu wa zamani Matata Ponyo; Georges Kapiamba, kutoka mashirika ya kiraia, anaomba kuachiliwa kwake mara moja. 

Mamlaka bado haijatoa taarifa yoyote kuhusu sababu za kukamatwa kwa mwanasiasa huyo wa upinzani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.