Pata taarifa kuu

Sudan: Watu 391 wafariki kutokana na Kipindupindu na Dengue

Jumla ya watu 391 wamekufa kutokana na Kipindupindu na ugonjwa wa Dengue katika mwaka wa vita nchini Sudan, Wizara ya Afya ya Sudan ilitangaza siku ya Alhamisi.

Kwa mujibu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA), mwaka mmoja baada ya kuzuka kwa mzozo kati ya Jeshi la Sudan (SAF) na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF), mnamo Aprili 15, 2023, Sudan inakabiliwa na moja ya majanga yanayoendelea kwa kasi duniani, yenye mahitaji ambayo hayajawahi kushuhudiwa.
Kwa mujibu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA), mwaka mmoja baada ya kuzuka kwa mzozo kati ya Jeshi la Sudan (SAF) na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF), mnamo Aprili 15, 2023, Sudan inakabiliwa na moja ya majanga yanayoendelea kwa kasi duniani, yenye mahitaji ambayo hayajawahi kushuhudiwa. AP
Matangazo ya kibiashara

Takriban wagonjwa 11,000 wa Kipindupindu walirekodiwa, vikiwemo vifo 325 katika Wilaya 12, huku wagonjwa wa homa ya Dengue wakifikia 9,000, vikiwemo vifo 66, Waziri wa Afya wa Sudan Haitham Mohamed Ibrahim alisema katika taarifa yake.

Licha ya mzozo huo, uingiliaji kati wa haraka unaofanywa na Wizara ya Afya umesaidia kuzuia kuenea kwa magonjwa ya mlipuko, kilisisitiza chanzo hicho, kikibainisha uagizaji wa vifaa vya matibabu vya haraka vya thamani ya pauni bilioni 19 za Sudan.

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kanda ya Mashariki ya Mediterania, Hanan Hassan Balkhi, alionya kwamba hospitali za Sudan ziko katika hatihati ya kukabiliwa na "uhaba wa dawa" wakati ambapo magonjwa ya milipuko yanaenea nchini humo.

Kati ya 70% na 80 ya hospitali katika Wilaya zilizoathiriwa na mzozo hazifanyi kazi, kutokana na mashambulizi ya muda mrefu, ukosefu wa vifaa vya matibabu, au ukosefu wa wafanyakazi wa afya, alisema.

Kwa mujibu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA), mwaka mmoja baada ya kuzuka kwa mzozo kati ya Jeshi la Sudan (SAF) na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF), mnamo Aprili 15, 2023, Sudan inakabiliwa na moja ya majanga yanayoendelea kwa kasi duniani, yenye mahitaji ambayo hayajawahi kushuhudiwa.

Takriban watu milioni 25, wakiwemo zaidi ya watoto milioni 14, wanahitaji msaada wa kibinadamu na usaidizi, na zaidi ya watu milioni 8.6, sawa na asilimia 16 ya watu wote nchini humo, wamekimbia makazi yao tangu kuanza kwa vita, inabainisha. OCHA

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.