Pata taarifa kuu
TANZANIA-MAGUFULI

Waziri Mkuu wa Tanzania, asema Magufuli yupo salama anaendelea na majukumu yake

Baada ya kutoonekana hadharani kwa wiki mbili na kuwepo kwa uvumi  kwenye mitandao ya kijamii kuwa rais wa Tanzania John Magufuli anaumwa, Waziri Mkuu wa nchi hiyo Kassim Majaliwa amesema rais Magufuli yupo salama na anaendelea na majukumu yake kama kawaida.

Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa Mwananchi
Matangazo ya kibiashara

Akizungumza siku ya Ijumaa, Majaliwa alisema kulikuwa na upotoshaji mkubwa kuhusu  juu ya afya na alipo rais Magufuli katika siku za hivi karibuni huku watu kwenye mitandoa ya kijamii ndani nan je ya nchi hiyo wakiendelea kuuliza aliko rais huo aliyechaguliwa tena kwa muhula wa pili mwezi Oktoba mwaka uliopita.

Katika hili nataka kuonesha masikitiko yangu kwa baadhi ya watanzania ambao hawapendi maendeleo ya taifa letu wamejaa na chuki tu, wako nje ya nchi na wanatamani kuwachonganisha watanzania.

Aidha, Majaliwa amesema wanaomzushia ugonjwa rais Magufuli wanaongozwa na chuki.

Tangu juzi mpaka leo asubuhi tunaona watanzania wenzetu wenye husda wanashawishi vyombo vya kimataifa wasema rais wa Tanzania anaumwa, kajifungia, tena hata hawapo Tanzania wapo nje. Sisi tupo ndani lakini tupo kimya. Wanaona fahari kuisema nchi yao vibaya.

Soma zaidi hapa-Rais Magufuli yuko wapi ? Wapinzani nchini Tanzania wauliza

Mara ya mwisho kwa Magufuli kuonekana hadharani ilikuwa ni Februari 27 wakati akimwapisha Katibu Mkuu kiongozi na hata hakuonekana wakati wa kikao cha viongozi wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, kilichofanyoka kupitia njia ya mtandao.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.