Tanzania yamuaga Magufuli Dodoma
Mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania John Magufuli unaagwa leo katika mji mkuu wa nchi hiyo Dodoma na viongozi mbalimbali kutoka barani Afrika na wananachi.
Imechapishwa:
Asubuhi hii, mwili wa Magufuli unaagwa na wabunge, kabla ya kuelekea katika uwnaja wa Michezo wa Jamhuri ambako ataagzwa rasmi na viongozi mbalimbali ambao wameanza kuwasili nchini humo. Leo ni siku ya mapumziko nchini humo.
Maelfu ya wananchi walijitokeza usiku wa kuamkia leo katika mji mkuu wa Tanzania Dodoma kuupokea mwili wa aliyekuwa rais wao Dkt John Pombe Magufuli aliyefariki tarehe 17.03.2021.
Marais wa nchi 10 na viongozi wengine wanatarajiwa kuhudhuria shughuli hiyo.
Magufuli ambaye alifariki dunia wiki iliyopita kufuatia matatizo ya moyo, atazikwa siku ya Ijumaa nyumbani kwake huko Chato.
Mwishoni mwa juma lililopita, maelfu walijitokeza jijini Dar es salaam kutoa heshima zao za mwisho.