Papa Francis ameongoza maombi kwa ajili ya waathiriwa wa shambulio nchini Uganda
NAIROBI – Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis, ameongoza maombi mjini Vatican kwa ajili ya waathiriwa wa shambulio la kigaidi kwenye shule mmoja nchini Uganda.
Imechapishwa:
Karibia watu 40-wengi wao wakiwa ni wanafunzi, waliripotiwa kuawaua kwa kukatwa kwa mapanga, kupigwa risasi na kuchomwa moto katika mji wa Magharibi wa Mpondwe Ijuma usiku.
Jeshi la Uganda limesema kuwa linawasaka waasi wa kundi la ADF wanaotuhumiwa kwa kutekeleza shambulio hilo ambalo limekashifiwa vikali kote duniani.
Nous prions aussi pour les jeunes étudiants, victimes de l'attaque brutale d'une école dans l'ouest de l'Ouganda. Persévérons dans la prière pour la population de l'Ukraine tourmentée, n'oublions pas qu'elle souffre tant. Prions pour la paix!
— Pape François (@Pontifex_fr) June 18, 2023
Kando na kutekeleza mauaji hayo, waasi hao wanaoendeleza shughuli zao mashariki mwa DRC, wametuhumiwa kwa kuwateka wanafunzi sita kabla ya kuvuka mpaka na kuingia nchini DR Congo.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni, amelaani shambulio hilo ambalo amelitaja kuwa la kioga.
Kwa mujibu wa rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ameagiza kutumwa kwa wanajeshi zaidi katika mpaka wa nchi hiyo na DRC, baada ya shambulio la hilo.
Fellow Ugandans, especially the Bazzukulu.
— Yoweri K Museveni (@KagutaMuseveni) June 18, 2023
Greetings. Condolences on the death of the 37 students of Nyabugaando Peter Hunter Secondary School at the hands of the terrorists of ADF, possibly working with other criminals, because I hear that school had some wrangles about it. I… pic.twitter.com/UmTkP7NmLo
Aidha katika taarifa yake, rais Museven, amehoji ilikuwaje jeshi lake lililoko nchini DRC lilishindwa kubaini mtego wa kundi hilo. Matamshi yake yalifuatia yale yaliyotolewa na mke wake Janet Museveni.
Tayari jeshi limesema linawashikilia watu kadhaa kwa mahojiano, wakati huu wakijaribu kubaini ni watu wangapi waliotekwa nyara na kundi hilo ingawa idadi ya awali ni watu 6 wakati huu baadhi ya familia zikianza kuwachukua wapendwa wao.