Uganda: Watu 20 wafariki katika ajali ya boti
Watu 20 wamethibitishwa kufariki baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama maji kwenye Ziwa Victoria nchini Uganda, ajali iliyotokea maajira ya saa tano asubuhi ya leo.
Imechapishwa:
Boti hiyo ilikuwa na watu 34 na ilikuwa ikitokea kisiwa cha Bukasa kuelekea Entebbe, ambapo polisi wanasema watu 9 wameokolewa, huku chanzo cha ajali hiyo kimethibitishwa kuwa ni upakiaji kupita kiasi na hali mbaya ya hewa
Kwa mujibu wa maofisa wa polisi nchini humo, boti hiyo ambayo ilikuwa imejaa kupita kiasi, ilikuwa pia imebeba magunia ya makaa, chakula na bidhaa nyengine.
#PRESSEELEASE |
— Uganda Police Force (@PoliceUg) August 2, 2023
Police Update on marine accident
On 2nd August 2023, a boat capsized on Lake Victoria.
The number of people on board are allegedly to be 34.
The incident happened at 5am. So far 20, people have been confirmed dead, and nine (9) rescued.
The boat was carrying… pic.twitter.com/bnHn4eOAca
Polisi wanasema ajali hiyo ilisababisha na hatua ya wahudumu wa boti hiyo kujaza watu na mizigo kupita kiasi, hali mbaya ya anga pia ikitajwa kuwa chanzo na kuzama kwa chombo hicho.
Maofisa wa uokoaji wakiwemo polisi na wanaheshi walikuwa wakiendelea na shughuli za kujaribu kuwatafuta watu waliotoweka. Ajali za boti sio kawaida nchini Uganda.
Mwaka wa 2020, karibia watu 26 walifairiki katika Ziwa Albert kwenye mpaka wa Uganda na Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
Miaka miwili kabla, watu wengine walithibitishwa kufariki baada ya boti iliyokuwa imewabeba karibia watu 100 kuzama kwenye Ziwa Victoria karibu na jiji kuu la Kampala.