Pata taarifa kuu

Uganda: Mfalme wa Rwenzururu, Charles Wesley Mumbere arejea nyumbani

Nairobi – Mfalme wa kikabila nchini Uganda amerejea nyumbani kwa kukaribishwa kwa shujaa, miaka saba baada ya makumi ya watu kuuawa wakati wa uvamizi wa polisi kwenye ikulu yake.

Ufalme wa Rwenzururu ni wa watu wa kabila la Bakonzo na una historia ya mielekeo ya kujitenga na mivutano ya muda mrefu na serikali ya Uganda
Ufalme wa Rwenzururu ni wa watu wa kabila la Bakonzo na una historia ya mielekeo ya kujitenga na mivutano ya muda mrefu na serikali ya Uganda Wikimedia Commons
Matangazo ya kibiashara

Umati wa watu wenye shangwe ulijitokeza katika mitaa ya Kasese kwa ajili ya kumpokea mfalme wa Rwenzururu, Charles Wesley Mumbere.

Mnamo mwaka wa 2016 alishtakiwa kwa kuwaamuru wanamgambo kutoka katika Ikulu yake kwa lengo la kuunda serikali yake huru inayojisimamia.

Mfalme huyo amerejea Kasese kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka saba

Serikali ya Uganda ilisema zaidi ya watu 100 waliuawa wakati wa operesheni hiyo  ya polisi lakini mashirika ya kutetea haki ya binadamu yalisema watu wengi zaidi waliuawa.

Mfalme Mumbere na makumi ya wengine walikabiliwa na mashtaka kadhaa yakiwemo uhaini, mauaji na ugaidi lakini waendesha mashtaka walifuta kesi hiyo baada ya kuomba msamaha.

Ufalme wa Rwenzururu ni wa watu wa kabila la Bakonzo na una historia ya mielekeo ya kujitenga na mivutano ya muda mrefu na serikali ya Uganda.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.