Madaktari nchini Kenya wasitisha mgomo wa kitaifa baada ya siku 56
Chama cha Madaktari nchini Kenya kimetangaza kusitisha mgomo wa kitaifa ulioanza mwezi Machi, baada ya kutia saini mkataba na serikali Jumatano jioni jijini Nairobi baada ya mazungumzo ya siku kadhaa.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Hata hivyo, undani wa mkataba huo haujawekwa wazi lakini uongozi wa Madaktari umesema kuwa, umeafikia maamuzi hayo baada ya mashauriano ya muda mrefu katika Kamati kuu ya chama chao.
Madkatari hao walitaka nyongeza ya mshahara, kuboreshewa mazingira ya kufanya kazi na kulipwa kwa Madaktari wanafunzi kwa mujibu wa mkataba waliokuwa wamekubaliana na serikali iliyopita mwaka 2017, Shilingi za nchi hiyo 206,000.
It has been a real war. Doctors have stood strong to protect the profession. I am so very proud of you all. May God bless you and light a special light on your careers, families and everything. Tonight i will share every page of the Document that was signed. #DoctorsStrikeKE ends pic.twitter.com/eVuCipcszo
— Alenga Torosterdt (@MzalendoAlenga) May 8, 2024
Davji Attelah Katibu Mkuu wa chama cha Madaktari nchini humo amesema, baada ya mashauriano ya muda mrefu, wamekubali kutia saini mkataba wa kusitisha mgomo.
“Mgomo ulioanza Machi 13 2024 umefika mwisho. Madaktari watafika kazini ndani ya saa 24 zijazo,” alisema Attelah.
Kuhusu suala tata la Madaktari wanafunzi kulipwa mshahara waliotaka, muungano huo umesema mwafaka haujapatikana, lakini imekubaliwa kuwa mashaurinao zaidi yaendelee.
Naye Waziri wa afya, Susan Nakhumicha, amesema serikali imeridhika kuwa mgomo huo umefika mwisho.
“Nawashukuru Madaktari kwa kukubali kusitisha mgomo. Wagonjwa sasa wataendelea kutibiwa,” alisema.
On behalf of the National Government, Health Cabinet Secretary Hon. @Nakhumicha_S signed the deal, with witnesses including Head of Public Service @koske_felix, Labour Cabinet Secretary Hon. Florence Bore and Public Service Cabinet Secretary @HonMoses_Kuria, PS Medical Services… pic.twitter.com/SwhUvmiLHY
— Ministry of Health (@MOH_Kenya) May 8, 2024
Tangazo la kusitishwa kwa mgomo ni habari njema kwa wagonjwa ambao wamekuwa wakiteseka wanapokwenda kwenye hospitali za umma kupata huduma za afya.
Baada ya hatua hii, Wakenya wanasubiri kuona namna mkataba huo utakavyotekelezwa.