Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii
Kenya, Uganda na Tanzania kuandaa Afcon 2027, Tshisekedi asema uchaguzi utafanyika tu
Imechapishwa:
Cheza - 20:13
Katika makala hii tumeangazia baadhi ya habari kuu za dunia za wiki hii na miongoni ni pamoja na Kenya, Uganda na Tanzania ziliteuliwa na shirikisho la soka Afrika CAF kuwa wenyeji wa mashindano ya kombe la Afrika mwaka 2027, DRC na Rwanda ziligubika mkutano wa Baraza la Umoja wa mataifa, balozi wa Ufaransa nchini Niger Sylvain Itté aliongea kwa mara ya kwanza kuhusu namna alivyofurushwa Niamey, Siasa za Marekani Israeli na kwengineko duniani ni miongoni mwa mengi tumekuandalia