Wananchi wa Tanzania wapigwa na butwaa kufwatia kugundulika kwa mifunko ya viungo vya binadamu
Imechapishwa:
Cheza - 21:47
Ni wiki ambayo wananchi wengi nchini Tanzania walipigwa na butwaa baada ya kugundulika kwa mabaki ya viungo vya binadamu, mjini Daresalaam ambapo polisi ilibainisha kuanzisha uchunguzi kubaini wahusika na kuahidi kutoa maelezo zaidi wakati mwafaka.Huko Mali kulipatikana mabaki ya ndege ya Algeria iliyoanguka ikiwa na abiria 116 miongoni mwao 51 wakiwa ni raia wa Ufaransa, wakati nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo kwa juma hili, serikali ilizindua rasmi kampeini ya kuwaelezea wananchi sababu ya kuwahamishia waasi wa Rwanda wa FDLR katika mji wa Kisangani mashariki mwa nchi hiyo. Pia katika makala haya tunaangazia hatua ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitishwa kwa mashambulizi ya ukanda wa Gaza na majeshi ya Israeli kwa masaa 12 pekee kufwatia masuala ya kibinadamu.Ungana nami Reuben Lukumbuka, karibu....