CAR: viongozi wa kidini wayashushia lawama makundi ya Seleka na Anti-balaka
Maaskofu wa makanisa mbalimbali nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, wameyatuhumu makundi ya Seleka na Anti-Balaka kuwa chanzo cha kuendelea kuzorota kwa hali ya usalama kwenye taifa hilo ambalo linakabiliwa na changamoto ya mauji ya kidini.
Imechapishwa:
Cheza - 01:45
Maaskofu hawa wanadai kuwa makundi kama vile ya Seleka, Anti-Balaka, Fulani na kundi la LRA la nchini Uganda yamekuwa yakijichukulia sheria mkononi kwa kutekeleza mauaji dhidi ya raia wanaowakamata.
Licha ya sehemu kubwa ya mauaji ya kiholela kudhibitiwa mjini Bangui, bado maeneo mbalimbali ya nchi yemeendelea kushuhudia uwepo wa matukio ya unyanyasaji, mateso na mauji dhidi ya raia yanayofanywa na makundi haya, ambapo viongozi wa dini sasa wanataka makundi hayo kukomesha vitendo vya kikatili.
Wachambuzi wa mambo wanasema kauli hii ya maaskofu ni ya kupongezwa, kwani makundi haya ya Seleka na Anti-balaka hayana nguvu, bali chuki kati ya raia nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati imepandikizwa kidini.