Pata taarifa kuu

DRC: Mapigano yaendelea kurindima karibu na Goma

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wanajeshi wa serikali na waasi wa M23 wameendelea kupambana karibu na mji wa Goma, katika jimbo la Kivu Kaskazini, huku mjumbe wa amani kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, rais wa zamani wa Kenya, Uhuru Kenyatta akitoa wito kwa makundi ya waasi kuweka silaha chini. 

Mapigano mashariki mwa DRC yamewapa motisha mamia ya watu wanaojitolea kujiunga na vita dhidi ya waasi wa M23. Hapa, watu wakiojitolea kujiunga na jeshi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Goma, Novemba 14, 2022.
Mapigano mashariki mwa DRC yamewapa motisha mamia ya watu wanaojitolea kujiunga na vita dhidi ya waasi wa M23. Hapa, watu wakiojitolea kujiunga na jeshi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Goma, Novemba 14, 2022. © Guerchom Ndebo / AFP
Matangazo ya kibiashara

Ripoti zinasema mapigano makali tangu hapo jana yamekuwa yakishuhudiwa katika êneo la Kibumba, karibu Kilomita 20 kutoka mji wa Goma. 

Aidha, ripoti zingine za kiusalama zimesema waasi wa M 23 wameonekana katika mbunga ya  taifa ya Virunga. 

Wakati mapigano hayo yakiendelea, na kuwapa wasiwasi wakaazi wa Kivu Kaskazini hasa mjini Goma, mjumbe kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, rais wa zamani wa Kenya Uhuru Kenyatta  amemaliza ziara yake ya siku mbili jijini Kinshasa, kuelekea mazungumzo ya amani wiki ijayo jijini Nairobi. 

Wakazi wa Mashariki wma DRC, wanasubiri kuona iwapo juhudi hizi za kidiplomazia zitasaidia na kuzaa matunda ya kuleta utulivu Mashariki mwa nchi yao. 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.