Pata taarifa kuu
MAREKANI-FERGUSON-MAANDAMANO-Usalama

Marekani: Baadhi ya miji yakumbwa na machafuko

Zaidi ya wanajeshi elfu 2 wamepelekwa kwenye mji wa Ferguson nchini Marekani ambako maelfu ya raia wanaandamana kupinga uamuzi wa jupu la wanasheria kwenye mahakama mjini humo.

Raia huyu mkaazi wa california akivaa bendera ya Marekani wakati wa maandamano katika mji wa Oakland (California) akidai haki kwa Michael Brown, kijana mweusi aliyeuawa kwa kupigwa risasi sita na polisi, Agosti 9 mwaka 2014 katika mji wa Ferguson.
Raia huyu mkaazi wa california akivaa bendera ya Marekani wakati wa maandamano katika mji wa Oakland (California) akidai haki kwa Michael Brown, kijana mweusi aliyeuawa kwa kupigwa risasi sita na polisi, Agosti 9 mwaka 2014 katika mji wa Ferguson. REUTERS/Elijah Nouvelage
Matangazo ya kibiashara

Waandamanaji hao wamelituhumu jopu hilo kushindwa kumfungulia kesi polisi anayedaiwa kumuua Michael Brown kijana mwenye asili ya kiafrika.

Mamia ya wananchi wameendelea kukabiliana na polisi kwenye mji huo pamoja na miji mingine ya marekani wakipinga uamuzi huu wanaodai umekwenda kinyume na matakwa ya sheria, huku wanaharakati wa kutetea haki za binadamu akiwemo mwanaharakati mkongwe Al Sharpton wakilaani uamuzi uliotolewa kuhusu kesi hii.

Kwa upande wake mwanasheria wa familia ya Michael Brown, Benjamin Crump, amesema kuwa uamuzi huu haukuzingatia haki licha ya ushahidi wa kutosha aliouwasilisha kwa jupo hilo la wanasheria.

Rais Barack Obama ameendelea kutoa wito kwa wakaazi wa mji wa Ferguson kujiepusha na vurugu ikiwemo kuchoma moto magari na kufanya vitendo vya uporaji akiahidi kuwa watu waliohusika na vurugu hizo watachukuliwa hatua za kisheria.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.