Chelsea yatoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Liverpool
Nchini Ungereza, klabu ya soka ya Chelsea, ilitoka nyuma baada ya kufungwa mabao mawili na Liverpool na kulazimisha sare ya mabao mawili kwa mawili, katika mechi ya kuvutia ya ligi kuu nchini humo, Jumapili usiku.
Imechapishwa:
Liverpool ilianza kutikisa nyavu katika dakika ya 9 kipindi cha kwanza, baada ya mshambuliaji wake Sadio Mane kuipa timu yake uongozi, na baadaye Mo Sala kufunga la pili katika dakika ya 26 ya mchuano huo.
Hata hivyo, dakika 3 kabla ya mapumziko, Mateo Kovačić aliifungia Chelsea baola kwanza, huku Christian Pulisic akifunga la pili dakika tatu baadaye na hadi mapumziko, timu zote zilikuwa zinatoshana nguvu.
Matokeo mengine
Brentford 2-1 Aston Villa
Everton 2-3 Brington
Leeds 3-Burnley.
Leo
Manchester United watamenyana na Wolvehampton Wanderer saa Mbili na nusu usiku