Pata taarifa kuu
JAPANI-JORDAN-MATEKA-IS-USALMA

Abe alaani kitendo cha utekaji nyara cha IS

Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe amelaani onyo la kundi la Islamic State kutishia kumuua Kenji Goto, mateka raia wa Japan wanayemshikilia.

Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe, akisononeshwa na kutekwa nyara kwa raia wake na kundi la wapiganaji wa Dola la Kiislamu.
Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe, akisononeshwa na kutekwa nyara kwa raia wake na kundi la wapiganaji wa Dola la Kiislamu. REUTERS/Issei Kato
Matangazo ya kibiashara

Kundi la wapiganaji ewa Dola la Kiislamu limetoa muda wa saa 24 zijazo kwakata vichwa mateka ho iwapo serikali za nchi hizo mbili hatotekeleza masharti lililoyatoa.

Islamic State inasema, Bwana Goto na Rubani kutoka Jordan watauawa kwa kukatwa kichwa ikiwa nchi ya Jordan haitamwachilia huru mwanamke mmoja aliyehukumiwa kifo.

Waziri Mkuu Abe, amesema serikali yake inashirikiana na Jordan kuhakikisha kuwa mateka hao wanaachiliwa huru.

Jumapili iliyopita, Islamic State ilimuua kwa kumkata kichwa mateka mwingine wa Japan Haruna Yukawa.

Awali kundi la wapiganaji wa Dola la Kiislamu lilidai serikali ya Japani fidia ya dola milioni 200 kwa ajili ya kuokoa maisha ya raia wake waili lililokua likiwashikilia mateka. Kundi hilo lilitoa masaa 72 kwa serikali ya Japani ili iwe imeshalipa pesa hizo.

Tokyo haikuchelewa kujibu, ikithibitisha kwamba haitashinikizwa wala kutishwa na ugaidi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.