Pata taarifa kuu

Marekani yakubali kuondoa kikosi chake cha kupambana na wajihadi Niger

Maafisa kadhaa wa Marekani wamethibitisha kuwa wanajeshi zaidi ya elfu moja wanaoshiriki katika vita dhidi ya ugaidi wataondoka Niger, baada ya kushtumiwa kwa makubaliano ya ushirikiano na utawala wa kijeshi huko Niamey.

[Picha ya zamani] Katika picha hii iliyopigwa Aprili 16, 2018, bendera za Marekani na Niger zinapandishwa bega kwa bega katika kambi ya wanajeshi wa anga huko Agadez.
[Picha ya zamani] Katika picha hii iliyopigwa Aprili 16, 2018, bendera za Marekani na Niger zinapandishwa bega kwa bega katika kambi ya wanajeshi wa anga huko Agadez. AP - Carley Petesch
Matangazo ya kibiashara

Na mwanahabari wetu nchini Marekani, David Thomson

Ombi la kujiondoa lilikubaliwa rasmi na nambari mbili katika diplomasia ya Marekani wakati wa mkutano huko Washington na Waziri Mkuu wa Niger. Kwa mujibu wa makubaliano haya, ujumbe wa Marekani utasafiri kwa ndege hadi Niger katika siku zijazo ili kupanga maelezo ya kuondoka kutoka Niger kwa askari hawa zaidi ya elfu moja wa Marekani wanaohusika katika mapambano dhidi ya makundi ya wanajihadi katika ukanda wa Sahel. Marekani tayari imesitisha ushirikiano wake mwingi na Niamey kufuatia mapinduzi ya Julai 26.

Mwezi Machi, Niger ilishutumu makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi yaliyotiwa saini na Marekani mwaka 2012, ikibaini kwamba yaliwekwa kwa upande mmoja na Washington. Tangu kuchukua madaraka, utawala mpya wa Niamey umejitia karibu na Urusi kama vile Mali na Burkina Faso. Katikati ya mwezi wa Januari, Moscow ilitangaza hitimisho la makubaliano yenye lengo la kuimarisha ushirikiano wake wa kijeshi na Niamey.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.