Pata taarifa kuu
MAREKANI-BALTIMORE-MAANDAMANO

Marekani: maandamano mapya yatokea Baltimore

Maandamano mapya yametokea katika mji wa Baltimore nchini Marekani kufuatia kifo cha Freddie Gray, kijana mweusi aliyefariki kutokana na majeraha akiwa mikononi mwa polisi.

Polisi ikiwakamata waandamanaji baada ya mazishi ya kijana mweusi Freddie Gray, Baltimore, April 27 mwaka 2015.
Polisi ikiwakamata waandamanaji baada ya mazishi ya kijana mweusi Freddie Gray, Baltimore, April 27 mwaka 2015. REUTERS/Sait Serkan Grubs
Matangazo ya kibiashara

Raia wengi wameingia mitaani, wakionyesha ujasiri wao licha ya hali mbaya ya hewa iliyoripotiwa katika mji huo.

Awali maelfu ya watu waliandamana katika miji mikubwa nchini Marekani kushinikiza polisi kuacha kuwanyanyasa watu wenye asili ya Afrika.

Maandamano hayo yalifanyika baada ya kijna mmoja mwenye asili ya Kiafrika kuuawa alipokuwa anazuiliwa na polisi katika mji wa Baltimore katika jimbo la Maryland juma lililopita.

Katika mji wa Baltimore waandamanaji waliokuwa na hasira walihakikisha kuwa shughuli zote zinasimama wakati wa maandamano hayo.

Miji ambayo imeshuhudia maandamano hayo mbali na Baltimore ni pamoja na New York, Boston na jiji kuu la Washington DC.

Maandamano ya Alhamisi wiki hii yaliekuwa ya amani katika miji yote.

Siku tatu zilizopita katika mji wa Baltimore polisi walikabiliana na waandamanaji ambao waliamua kupora na kuvamia watu baada ya kuawa kwa kijana huyo mweusi.

Matokeo ya mwanzo ya uchunguzi wa polisi wa jinsi kijana wa miaka ishirini na mitano mwenye asili ya weusi alivyouawa bado hayajawekwa hadharani.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.