Muungano wa Indo-Pacific: baada ya Korea Kusini, Joe Biden atarajiwa Japani
Rais wa Marekani Joe Biden anawasili Tokyo Jumapili hii baada ya kukaa zaidi ya siku mbili nchini Korea Kusini ili kuthibitisha ahadi ya Marekani ya kumtetea mshirika wake wa Korea Kusini dhidi ya Korea Kaskazini na kusisitiza haja ya kudumisha "huru na wazi" wa ukanda wa Indo-Pacific.
Imechapishwa:
Rais wa Marekani anakuja Tokyo kushiriki katika mkutano wa kilele wa Quad siku ya Jumanne, unaoleta pamoja Marekani, Japan, India na Australia.
Kwa mujibu wa Rais Joe Biden, muungano wa Quad lazima usaidie kuzuia kujiimaisha kwa China katika eneo la Indo-Pasifiki, ikizingatiwa hatari ya uvamizi wa China kwa Taiwan na kuongezeka kwa luteka za kijeshi kati ya China na Urusi katika ukanda huo.
Huko Tokyo, muungano huu usio rasmi utaongeza programu ya kiuchumi kwenye mfumo wake wa usalama kwa sababu ya matatizo na India kuhusu masuala ya ulinzi. Marekani itazindua kundi jipya la kiuchumi, lililo wazi kwa nchi za eneo la Indo-Pasifiki, linalonuiwa kuunganisha mazingira, biashara, viwango vya kidijitali na kuanzisha mfumo wa ugavi bila China.