Pata taarifa kuu

Mkutano wa baraza la mazingira unaendelea jijini Nairobi

Nairobi – Mawaziri wa mazingira na wadau mbambali kutoka zaidi ya nchi 180 wanakutana jijini Nairobi nchini Kenya, kwenye mkutano wa sita wa Umoja wa Mataifa kuhusu mazingira UNEA, kujadili namna ya kuendelea kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Zaidi ya wajumbe 7,000 wanaudhuria mkutano wa mazingira jijini Nairobi.
Zaidi ya wajumbe 7,000 wanaudhuria mkutano wa mazingira jijini Nairobi. © UNEA
Matangazo ya kibiashara

Huku athari za mabadiliko ya hali ya hewa zikiendelea kuongezeka duniani, uchafuzi wa mazingira umeonekana kuwa sababu kuu ya vifo vya mapema duniani.

Waziri wa mazingira nchini Kenya, Soipan Tuya.
Waziri wa mazingira nchini Kenya, Soipan Tuya. © Soipan Tuya

Watetezi wa mazingira sasa wanayataka  mataifa kuzingatia zaidi sheria za mazingira ili kujikwamua kutoka kwa athari hizi.  Leila Benali ni rais wa baraza la mazingira la Umoja wa Mataifa.

“Tuko katika wakati ambapo tunahitaji kurejesha imani miongoni mwa mataifa na imani katika ubinadamu na kile kilichosalia kwetu katika utu wa kuboresha mazingira.” alisema Leila Benali ni Rais wa baraza la mazingira la umoja wa mataifa.

00:10

Leila Benali ni Rais wa baraza la mazingira la umoja wa mataifa

Tayari malengo 19 yamependekezwa kwenye mkutano wa baraza la mazingira unaondelea jijini Nairobi,malengo hayo yakijumuisha uimarishaji wa kawi safi,kupunguza matumizi ya kemikali na kuangazia utaratibu wa kuchakata taka (Recycling.)

Kongamano kuhusu mazingira linaendelea jijini Nairobi
Kongamano kuhusu mazingira linaendelea jijini Nairobi © Soipan Tuya

Inger Andersen ni Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la umoja wa mataifa kuhusu mazingira.

 “Ni muhimu sana kwamba ulimwengu wote unajizatiti kuchukua hatua kuhusu mazingira, ili tuweze kukidhi malengo endelevu ambayo tuliahidi kila mmoja wetu mwaka 2015.”Inger Andersen ni Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la umoja wa mataifa kuhusu mazingira.

00:14

Inger Andersen ni Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la umoja wa mataifa kuhusu mazingira

Hata hivyo mashirika ya mazingira nayo yanaendelea kushinikiza wajumbe kupea teknolojia kipau mbele kuhepuka matumizi ya mafuta ya kisukuku ambayo yamechangua pakubwa uharibifu wa mazingira. Hawa ni baadhi ya watetezi wa mzingira.

00:18

Wanaharakati wa Mazingira nchini kenya

Zaidi ya wajumbe 7,000 wanaudhuria mkutano huo wa mazingira jijini Nairobi Kauli mbiu ikiwa hatua za kimataifa zenye ufanisi, na endelevu kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Victor Moturi- RFI Kiswahili, Nairobi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.