Pata taarifa kuu
MASHARIKI YA KATI-ASIA-UGAIDI-Usalama

Makundi ya kislamu yaaendelea kujidhatiti

Wakati jeshi nchini Nigeria likiongeza mashambulizi zaidi kukabilia na wapiganaji wa kiislamu wa Boko Haram ambao wameendelea kuhatarisha usalama nchini humo, ripoti mpya zinaonesha kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa la makundi ya kiislamu kwenye ukanda wa mashariki ya kati hadi Asia.

Wapiganaji wa kundi la Boko Haram Boko Haram.
Wapiganaji wa kundi la Boko Haram Boko Haram. AFP PHOTO/YOUTUBE
Matangazo ya kibiashara

Ripoti hiyo inasema kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa la makundi haya ya kiislamu kayika kipindi cha miezi 12 iliyopita kutokana na vita nchini Syria na mashambulizi ya Boko Haram nchini Nigeria, shirika la kimataifa la utafiti la Pew limesema kwenye ripoti yake.

Askari polisi wa Nigeria wakiendesha operesheni ya kuwasaka wapiganaji wa kundi la Boko Haram, katika mji wa Maiduguri, jimboni Borno, nchini Nigeria.
Askari polisi wa Nigeria wakiendesha operesheni ya kuwasaka wapiganaji wa kundi la Boko Haram, katika mji wa Maiduguri, jimboni Borno, nchini Nigeria. AFP PHOTO / Quentin Leboucher

Ripoti hii inasema kuwa makundi ya Al-Qaeda, Hezbollah, Boko Haram na hata kundi la Hamas ambalo limeshinda hata kwenye uchaguzi wa Palestina yameanza kupoteza uungwaji mkono na makundi haya.

Wachambuzi wa masuala ya usalama na siasa wanasenasema makundi haya ya kislamu yanaonekana kuwa yanafadhiliwa kimataifa na kundi la Al Qaeda, huku wakibaini kwamba makundi hayo huenda yana mafungamano na kundi hilo la Al Qaeda.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.