Pata taarifa kuu

Abbas aitaka Marekani kushawishi Israel kutothubutu kushambulia Rafah

Rais wa Mamlaka ya Palestina Mahmoud Abbas, ameitaka Marekani kusaidia, kwa kuizuia mpango wa jeshi la Israeli kuvamia mji wa Rafah kwa kutuma vikosi vyake vya ardhini.

Kiongozi wa mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas, katika mji wa Ramallah.
Kiongozi wa mamlaka ya Palestina, Mahmoud Abbas, katika mji wa Ramallah. AFP - JAAFAR ASHTIYEH
Matangazo ya kibiashara

Kiongozi huyo wa Palestina amesema iwapo Israel itavamia mji wa Rafah, itakuwa ni janga kubwa sana kwenye historia ya raia wa Palestina, na Marekani ndio nchi pekee yenye uwezo wa kuzuia mpango huo wa mshirika wake Israeli.

Aidha, rais Abbas amesema anahofia kuwa wanajeshi wa Israeli wanapanga kuushambulia ukingo wa Magharibi, baada ya kumalizana na ukanda wa Gaza.

Katika hatua nyingine, Saudi Arabia inasema inataka uthabiti wa kikanda ikionya kuwa, vita vinavyoendelea kati ya Israeli na Hamas, ikisema inaharibu mshikamo wa nchi za kikanda.

Wakati hayo yakijiri, kiongozi wa juu wa kundi la Hamas Khalil al-Hayya amesema, kundi hilo litajibu mapendekezo ya Israeli kuhusu mpango wa kusitisha vita kwenye ukanda wa Gaza watakapokutana siku ya Jumatatu nchini Misri.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.