Pata taarifa kuu

Sevilla ndio mabingwa wa ligi ya Europa 2023

NAIROBI – Sevilla wameshinda taji la saba la ligi ya Europa baada ya kuwashinda Roma kwa mikwaju ya penalti kwenye uwanja wa Puskas Arena mjini Budapest.

Sevilla ya Uhispania ndiyo mabingwa wa  Europa msimu huu.
Sevilla ya Uhispania ndiyo mabingwa wa Europa msimu huu. AP - Petr David Josek
Matangazo ya kibiashara

Gonzalo Montiel, ambaye pia alifunga penalti ya ushindi kwa timu ya taifa ya Argentina katika fainali ya Kombe la dunia dhidi ya Ufaransa nchini Qatar, aliifungia klabu yake ya Uhispania kufuatia sare ya 1-1.

Roma ya  Uhispania, sasa imeshinda fainali zote saba walizocheza katika mashindano hayo huku nahodha Jesus Navas akishiriki katika ushindi wao wa kwanza dhidi ya Middlesbrough mnamo 2006.

Hatua hii inawafanya kufuzu kwa ligi ya mabingwa msimu ujao licha ya kumaliza nje ya nne bora kwenye La Liga.

Wachezaji wa klabu ya Sevilla ya Uhispania
Wachezaji wa klabu ya Sevilla ya Uhispania AP - Denes Erdos

Jose Mourinho kocha wa Roma  alikuwa ameshinda fainali zote tano za awali za Europa alizoshiriki. Paulo Dybala aliiweka Roma mbele katika kipindi cha kwanza. Nao Sevilla walisawazisha katika dakika ya 10 baada ya kipindi cha mapumziko. 

Wachezaji wa AS Roma baada ya mechi ya fainali ya Europa
Wachezaji wa AS Roma baada ya mechi ya fainali ya Europa AP - Darko Vojinovic

Roma bila shaka walipata fursa nzuri zaidi za kushinda mechi hiyo  katika muda wa kawaida huku Tammy Abraham na Ibanez wakikosa nafasi nyengi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.