Pata taarifa kuu
UKRAINE-DONETSK-LUGANSK-Uchaguzi_siasa

Mgogoro Ukraine: jeshi latumwa katika miji muhimu

Rais wa Ukraine Petro Poroshenko ameliamuru jeshi, kuimarisha usalama katika miji ya kusini na Mashariki mwa nchi hiyo kwa hofu ya kuzuka kwa uasi mpya.

wanajeshi watumwa kuimarisha usalama katika miji muhimu, ukiwemo mji wa Mariupol, Novemba 2 mwaka 2014.
wanajeshi watumwa kuimarisha usalama katika miji muhimu, ukiwemo mji wa Mariupol, Novemba 2 mwaka 2014. REUTERS/Nikolai Ryabchenko
Matangazo ya kibiashara

Rais Poroshenko ametaja miji inayostahili kupewa ulinzi mkali ni pamoja na Mariupol, Berdyansk, Kharkiv na Kaskazini mwa jimbo la Luhansk.

Kiongozi huyo wa Ukraine ametoa agizo hilo baada ya kukutana na viongozi wa usalama katika majimbo ya Donetsk na Luhansk yanayodhibitiwa na waasi.

Poroshenko pia amesisitiza kuwa serikali yake bado ina nia ya kutekeleza mpango wa amani ulioafikiwa mwezi Septemba mwaka huu mjini Minsk nchini Belarus ili kumaliza mzozo mashariki mwa nchi hiyo.

Katika hatua nyingine, amelaani uchaguzi uliotokea mashariki mwa nchi hiyo na kuungwa mkono na Urusi na kusisitiza kuwa ulikuwa kinyume na sheria.

Tayari viongozi wa majimbo ya Donetsk na Luhansk waliochaguliwa mwishoni mwa juma lililopita wameapishwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.