Pata taarifa kuu

Ufaransa umeitaka serikali ya Burundi kuadhibu watu wanaonyanyasa wengine

Nchi ya Ufaransa imeomba watu wote wanaonyanyaswa wengine kwa sababu za kisiasa nchini Burundi waadhibiwe bila upendelevu kwa lengo la kujiandalia chaguzi zenye haki mwaka 2015.

Baadhi ya askari polisi na baadhi ya wafuasi wa vyama vya kisiasa nchini Burundi wananyooshewa kidole kwa vitendo vya kuwanyanyasa raia.
Baadhi ya askari polisi na baadhi ya wafuasi wa vyama vya kisiasa nchini Burundi wananyooshewa kidole kwa vitendo vya kuwanyanyasa raia. AFP PHOTO/Esdras NDIKUMANA
Matangazo ya kibiashara

Hayo ni matamshi ya balozi wa Ufaransa nchini Burundi Guérit Van Rossoum alipokuwa akihotubia wageni katika maadhimisho ya nchi ya miaka 225 tangu mapinduzi ya tarehe 14 july 1789.

Alexis Sinduhije, kiongozi wa chama cha upinzani cha MSD, ambaye kwa sasa anaishi uhamishoni nje ya nchi.
Alexis Sinduhije, kiongozi wa chama cha upinzani cha MSD, ambaye kwa sasa anaishi uhamishoni nje ya nchi. Photo: Esdras Ndikumana/ AFP

Hayo yakijiri upinzani nchini Burundi umeilalamikia serikali ya rais Nkurunziza kutaka kuingilia mchakato wa kuchunguza jaribio la kumuuwa kinara wa upinzani Charles Nditije wa chama cha Uprona.

Hivi majuzi, Waziri wa Mambo ya Ndani amesema kuwa huenda suala la jaribio hilo likawa njama ya mpinzani mwenyewe, huku msemaji wa polisi nchini Burundi akisikika akisema kuwa uchunguzi huo unaweza ukawekwa tu kwenye kapu.

Katika mkutano na waandishi wa habari jana, Charles Nditije ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha UPRONA ametoa shutuma hizo na kusema kuwa lengo la kuingilia uchunguzi ni ishara tosha kuwa serikali imeshiriki katika jaribio hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.