NIGERIA-BOKO HARAM-USALAMA
Askari 24 wa Nigeria wajeruhiwa katika shambulio la Boko Haram
Jeshi la Nigeria linasema wanajeshi wake 24 wamejeruhiwa katika makabiliano na kundi la kigaidi la Boko Haram katika jimbo la Borno.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Ripoti zinasema kuwa kwa sasa wanajeshi hao wanatibiwa katika hospitali ya kijeshi mjini Maiduguri.
Wapiganaji wa Boko Haram waliwavizia na kuwavamia wanajeshi hao katika mji wa Kareto na kuzua makabiliano hayo makali.
Serikali ya Nigeria imekuwa ikisema inafanikiwa katika vita dhidi ya kundi hili.