Pata taarifa kuu

Kampuni ya gesi na mafuta TotalEnergies yapata pigo baada ya ufadhili kukatwa

Mashirika karibu 60 ya kiraia kutoka nchi mbalimbali zimetaka benki zote na wawekezaji kusitisha ufadhili wa miradi ya gesi na mafuta inayofanywa  na kampuni ya kifaransa ya TotalEnergies katika nchi mbali mbali mradi mkubwa ukiwa nchini Uganda.

Kampuni ya mafuta na gesi ya Ufaransa ya TotalEnergies inaonekana katika ghala la mafuta la TotalEnergies huko Mardyck, karibu na Dunkerque, wakati Ufaransa.
Kampuni ya mafuta na gesi ya Ufaransa ya TotalEnergies inaonekana katika ghala la mafuta la TotalEnergies huko Mardyck, karibu na Dunkerque, wakati Ufaransa. REUTERS - PASCAL ROSSIGNOL
Matangazo ya kibiashara

Mashirika hayo kupitia barua mbili zilizoandikiwa kwa benki na wawekezaji, yanataka wawekezaji kutotoa mikopo  au ufadhili wowote unaohusishwa na TotalEnergies, ambayo yanaishtumu kwa kuendelea na agenda ya kuharibu mazingira licha ya pingamizi kadhaa.

Mashirika hayo yanasema miradi ya Total inaenda kinyume na malengo ya kidunia ya  kudhibiti viwango vya joto hati nyuzi moja nukta tano.

Shirika moja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo la FORED ,lilosaini barua hiyo ,linasema mradi wa Uganda litawaathiri moja kwa moja raia wa DRC, ardhi husika imenyakuliwa kwao , utasababisha uvujaji wa mafuta katika ziwa  la Albert  na matumizi makubwa ya maji .

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.