Pata taarifa kuu

DRC: Waathiriwa wa vitendo vya ukatili wa Bosco Ntaganda kulipwa fidia

Nairobi – Mwishoni mwa juma lililopita, majaji katika mahakama ya kimataifa inayoshughulikia kesi za uhalifu wa kivita, ICC, walithibitisha waathiriwa wa vitendo vya ukatili wa Bosco Ntaganda nchini CDRC, watalipwa kiasi cha dola za Marekani milioni 30 kama fidia.

Waathiriwa wa vitendo vya Bosco Ntaganda kulipwa fidia na ICC
Waathiriwa wa vitendo vya Bosco Ntaganda kulipwa fidia na ICC ANP/AFP
Matangazo ya kibiashara

Alifahamika kama “The terminator” Ntaganda alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela mwaka 2019 na mwaka uliopita majaji wa mahakama hiyo waliagiza waathiriwa kulipwa dola milioni 30.

Hata hivyo maagizo hayo hayajaanza kutekelezwa kwa kile mahakama hiyo inasema inanya mapitio kuwabaini waathiriwa halisi wa vitendo vyake.

Mahakama inakadiria kuwa kuna waathiriwa zaidi ya elfu 7 na kwamba kila mmoja anatarajiwa kulipwa dola elfu 4.

Licha ya kuwa Ntaganda, ndio anapaswa kulipa kiasi hicho cha fedha, mahakama ilibaini uwa hana uwezo na badala yake kiasi hicho kitalipwa kutoka kwenye mfuko maalumu wa mahakama hiyo ya the hague.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.