Pata taarifa kuu

Uganda: Mahakama ya ICC yatoa fidia kwa waathiriwa wa vitendo vya waasi wa LRA

Nairobi – Mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita imetoa malipo ya fidia kwa waathiriwa katika kesi inayomhusisha kamanda wa zamani wa waasi wa Lord's Resistance Army, Dominic Ongwen, ambaye sasa amefungwa.

Ongwen alikuwa kamanda mkuu wa LRA, wanamgambo wa waasi waliokuwa wakiendesha shughuli zao kaskazini mwa Uganda kutoka 1987 kwa miongo miwili
Ongwen alikuwa kamanda mkuu wa LRA, wanamgambo wa waasi waliokuwa wakiendesha shughuli zao kaskazini mwa Uganda kutoka 1987 kwa miongo miwili © ICC-CPI
Matangazo ya kibiashara

Ongwen alikuwa kamanda mkuu wa LRA, wanamgambo wa waasi waliokuwa wakiendesha shughuli zao kaskazini mwa Uganda kutoka 1987 kwa miongo miwili.

Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita ya (ICC) ilimtunuku kila mwathiriwa, ambao idadi yao inakadiriwa kuwa 49,772, fidia ya Dola 800 za Marekani kila mmoja.

Hii ni rekodi ya $56 milioni kwa jumla, lakini waathiriwa hawatalipwa mara moja.

Mahakama ya ICC
Mahakama ya ICC REUTERS - Jerry Lampen

Baraza la uaminifu lilipewa jukumu la kukusanya pesa zinazohitajika kwa ajili ya fidia, huku jumuiya ya kimataifa ikialikwa kutoa michango. Mahakama pia ilitoa malipo ya pamoja kwa jamii.

Hizi zitazingatia mipango ya ukarabati inayolenga kurekebisha aina zote za uharibifu uliopatikana.

Dominic Ongwen alipatikana na hatia ya uhalifu wa kivita 61 na uhalifu dhidi ya ubinadamu na ICC mnamo Februari 2021.Uhalifu uliofanywa kati ya 2002 na 2005 ulijumuisha uhalifu wa kingono na kijinsia. Alihukumiwa kifungo cha miaka 25 jela.

Dominic Ongwen, alikuwa kiongozi wa waasi wa LRA nchini Uganda
Dominic Ongwen, alikuwa kiongozi wa waasi wa LRA nchini Uganda AFP - PETER DEJONG

Kamanda huyo wa zamani wa LRA alishiriki katika vita vilivyosababisha maelfu ya watu kuyahama makazi yao na kuwaacha mamia wakiwa wameuawa kaskazini mwa Uganda. Kwa sasa Ongwen anatumikia kifungo chake jela nchini Norway.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.