Pata taarifa kuu

EAC yakanusha madai ya kuzinduliwa kwa sarafu ya pamoja

Nairobi – Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imekanusha kutoa chapisho kwenye mtandao wa  kijalii wa X, kuwa nchi wanachama zimezindua  sarafu.

Mwaka 2013, nchi wanachama wa EAC ziliahidi kuzindua sarafu ya pamoja kufikia 2024 lakini mpango huo umeahirishwa hadi 2031.
Mwaka 2013, nchi wanachama wa EAC ziliahidi kuzindua sarafu ya pamoja kufikia 2024 lakini mpango huo umeahirishwa hadi 2031. © EAC
Matangazo ya kibiashara

Tangazo hili la EAC yenye makao yake jijini Arusha nchini Tanzania, limekuja baada ya kuwepo kwa chapisho mwishoni mwa wiki iliyopita, kwenye ukura wa X uliokuwa na jina la Government of East Africa.

Kwa mujibu wa taarifa kwenye akaunti hiyo ghusi,  sarafu hiyo ya pamoja imepewa jina la  East African Sheafra, ikijumuisha shilling ya Afrika Mashariki na Franca kutoka nchi za Rwanda, Burundi na DRC.

Akaunti pia ilichapisha picha ya noti bandia ya sarafu moja inayodaiwa kuwa kwenye mchakato wa kuzinduliwa.

Chapisho hili limepokea maoni zaidi ya Laki Tano, na lilisambazwa na baadhi ya vyombo vya habari na watu maarufu mtandaoni katika ukanda wa Afrika Mashariki.

EAC ilitupilia mbali ripoti ya kuwepo kwa sarafu ya kanda ya pamoja siku hiyo ya Jumapili, ikisema kwamba mchakato wa kuundwa kwa sarafu ya pamoja bado unaendelea.

Mwaka 2013, nchi wanachama wa EAC ziliahidi kuzindua sarafu ya pamoja kufikia 2024 lakini mpango huo umeahirishwa hadi 2031.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.