Uingereza yafuzu kucheza fainali ya Euro
Uingereza imefuzu fainali ya kuwania kombe la soka barani Ulaya, baada ya kuifunga Denmark mabao 2-1 katika mechi ya nusu fainali iliyochezwa jana usiku katika uwanja wa Wembley jijini London.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Denmark ilikuwa ya kwanza kupata bao katika dakika 30 kupitia mchezaji wake Mikkel Damsgaard, lakini Uingereza ikasawazisha dakika tisa baadaye baada ya Denmark kujifunga kupitia mchezaji wake Simon Kjaer.
Mpaka dakika 90, timu zote zilikuwa sare kwa bao moja kwa muda na kulazimu mechi hiyo kwenda mpaka muda wa ziada na ilipofika dakika ya 104, Harry Kane alikuwa shujaa wa timu yake baada ya kupachika bao la pili na la ushindi.
Uingereza sasa itamenyana na Italia katika ya fainali siku ya Jumapili.
😎 The EURO 2020 final is set!
— UEFA EURO 2020 (@EURO2020) July 7, 2021
🇮🇹🆚🏴 Italy versus England at Wembley Stadium on Sunday 🔥
Who is lifting the 🏆❓#EURO2020 pic.twitter.com/tYSEzNjAkI