Uganda: Kocha Masaba anamatumaini ya ushindi wakati BIDCO Limited ikiwa mgeni wa Wakiso Giants katika ligi
Nairobi – Kabla ya mechi ya ugenini dhidi ya Wakiso Giants, Kocha wa BUL Simeon Masaba ameonekana mwenye matumaini makubwa huku akitafuta ushindi wake wa kwanza tangu ajiunge na timu hiyo inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda.
Imechapishwa:
Mechi moja ya ligi kuu nchini Uganda itasakatwa leo alasiri. Wakiso Giants ambayo inashikilia nafasi ya 8 ikiwa na alama 31 baada ya mechi 24 itakuwa mwenyeji wa BUL katika uwanja wa Kabaka Kyabaggu.
BUL ni ya 7 kwenye jedwali ikiwa na alama 32 baada ya mechi 23.
Kocha mpya wa BUL Simeon Masaba bado hajapata ushindi tangu achukuwe nafasi ya kocha Alex Isabirye mwezi uliyopita.
Timu hizi mbili zinatofauti ya alama moja huku BUL ikiwa ana alama 32 ilhali Wakiso Giants ina alama 31.
Ratiba za mechi za ligi kuu nchini Uganda
Jumatatu Mei 1, 2023
- Wakiso Giants vs BUL – Kabaka Kyabaggu saa Kumi
Jumanne Mei 2, 2023
- KCCA vs Onduparaka – MTN Omondi uwanjani, Lugogo saa kumi
- Vipers vs Gaddafi – St. Mary’s stadium, Kitende saa moja jioni
Jumatano Mei 3, 2023
- Maroons vs SC Villa – Luzira Saa kumi
- Arua Hill vs Express FC – Barifa stadium, Arua saa kumi
- Blacks Power vs URA – Lira saa kumi
- Bright Stars vs Busoga United – Kavumba Recreation Ground saa nane
Ijumaa Mei 4, 2023
- Vipers SC vs KCCA – St. Mary’s stadium, Kitende saa moja