AFCON: Mechi za nusu fainali, DRC kucheza dhidi ya Ivory Coast
Nairobi – Michuano ya soka kuwania taji la mataifa ya Afrika, inachezwa leo Jumatano usiku.
Imechapishwa:
Mechi ya kwanza itakuwa kati ya Nigeria na Afrika Kusini, kuanzia saa Mbili usiku mjini Bouake.
Mataifa haya mawili yana ushindani wa muda mrefu katika mchezo wa soka.
Nyota wa Nigeria, Victor Osimhen ambaye wiki iliyopita alipata jeraha amepona na atacheza kwenye ya leo.
Mchezo huu pia umezua mvutano wa kidiplomasia, Balozi wa Nigeria nchini Afrika Kusini, amewaambia raia wa nchi yake kuwa makini leo usiku, iwapo wataishinda Afrika Kusini ili kuepuka sintofahamu inayoweza kutokea.
Katika hatua nyingine, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, nayo itacheza na wenyeji Ivory Coast jijini Abidjan.
Wachezaji wa Leopard katika mechi ya leo watavalia vitambaa vyeusi, kuomboleza na raia wengine wa nchi yao kutokana na mauaji ya watu huko Mashariki mwa DRC na kuomba amani.
Washindi wa mechi za leo, watakutana kwenye fainali siku ya Jumapili