Pata taarifa kuu
EBOLA-WHO-LIBERIA-GUINEA-SIERRA LEONE-Afya

Ebola: WHO yapongeza jitihada zinazoendeshwa na nchi mbalimbali

Shirika la afya duniani, WHO limetoa takwimu mpya kuonesha idadi ya watu waliopoteza maisha kutokana na ugonjwa hatari wa Ebola katika Mataifa ya Afrika Magharibi.

Madaktari na wauguzi nchini Liberia wakiendelea na zoezi la kuhamasisha raia juu ya maambukizi ya virusi vya Ebola, Julai 30 mwaka 2014.
Madaktari na wauguzi nchini Liberia wakiendelea na zoezi la kuhamasisha raia juu ya maambukizi ya virusi vya Ebola, Julai 30 mwaka 2014. Reuters/路透社
Matangazo ya kibiashara

WHO imesema idadi mpya ya watu waliopoteza maisha nchini Liberia , Guinea na Sireleon ni 4,818 wala sio 4,951 kama ilivyoripotiwa mwisho wa mwezi uliopita.

Shirika hilo limetoa pia takwimu mpya za maambukizi ambapo idadi imepungua kutoka watu 13,567 hadi 13,042.

Kati ya mataifa yaliyoathirika na Ebola, Liberia inaongoza kwa kuwa na watu wengi waliopoteza maisha ambao ni 2,697 huku 6,525 wakiwa wamelazwa wakiwa wamewekwa karantini, na inafuatwa na Sierra Leone, ambayo imepoteza watu 1,070.

WHO imesema sababu kubwa ya vifo kupungua ni jitihada zinazoendelea kuwahudumia wagonjwa wanaofika katika vituo vya afya kupata msaada.

Katika hatua nyingine, rais Barrack Obama amesema ataomba Bunge la Congress kupitisha mswada ili kuruhusu kutolewa kwa Dola bilioni 6 nukta 2 kusaidia kupambana na Ebola.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.