Pata taarifa kuu

Nchi tano zawasilisha malalamiko yao ICC kufuatia mashambulizi ya Israel katika eneo laPalestina

Nchi tano miongoni mwa nchi zilizotia saini kuhusu kuundwa kwa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) zimeomba kufanyika kwa uchunguzi kuhusu hali katika eneo la Palestina kufuatia mashambulizi ya Israel yanayoendelea.

Miili ya Wapalestina waliouawa na mashambulizi ya Israel katika ua wa hospitali ya Al-Shifa hapa ilikuwa tarehe 12 Novemba. Maafisa wa afya wanasema hawawezi kuwazika kwa sababu ya operesheni ya ardhini ya Israel.
Miili ya Wapalestina waliouawa na mashambulizi ya Israel katika ua wa hospitali ya Al-Shifa hapa ilikuwa tarehe 12 Novemba. Maafisa wa afya wanasema hawawezi kuwazika kwa sababu ya operesheni ya ardhini ya Israel. via REUTERS - AHMED EL MOKHALLALATI
Matangazo ya kibiashara

Hayo yametaganzwa na Mwendesha wa mahakaam hiyo, ambaye amebainisha kuchunguza kuhusu uhalifu uliofanywa tangu shamblio baya la hamas la Octoba 7 baada ya kupata malalamiko kutoka Afrika Kusini, Bangladesh, Bolivia, Comoro na Djibouti.

Afrika Kusini imeeleza kuwa imewasilisha malamiko haya na "nchi nyingine zinazotiwa wasiwasi na hali hii huko Palestina", ili ICC ichukuwe "hatua ya haraka kwa uzito wa hali ya sasa".

UNRWA yatangaza shambulio jipya la bomu kwenye mojawapo ya shule zake

Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA), Philippe Lazzarini amebainisha kwenye mtandao wa X (zamani ikiitwa Twitter) kwamba shule ya pili imelengwa, hii ni mara ya pili chini ya saa ishirini na nne. Shambulio la kwanza lilitokea katika kambi ya Jabaliya Jumamosi asubuhi.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.