COP28: Rasimu ya makubaliano ya 'mpito' kutoka kwa nishati ya mafuta
Rasimu mpya ya makubaliano katika mkutano kuhusu tabia nchi, COP28, huko Dubai inatoa wito kwa nchi "kuondokana na nishati ya mafuta" na kuharakisha hatua "katika muongo huu muhimu, ili kufikia hali ya kutoegemea upande wowote wa kaboni mnamo mwaka 2050", kulingana na maelewano ya hivi karibuni ambayo Falme za Kiarabu zitajaribu kuidhinisha kwa makubaliano Jumatano hii.
Imechapishwa:
Kutoka kwa mwandishi wetu maalum huko Dubai
Nakala hiyo, inayotarajiwa tangu Jumanne alasiri na kuchapishwa leo alfajiri huko Dubai, ambayo inalenga kuwa uamuzi wa kwanza wa mkutano wa tabia nchi wa Umoja wa Mataifa kushughulikia hatima ya nishati zote za mafuta - mafuta, gesi na makaa ya mawe - sio ndio sababu inayodaiwa na nchi zenye malengo makubwa zaidi lakini imekataliwa na nchi zinazozalisha bidhaa hizo, Saudi Arabia ikiongoza.
Hati hiyo sasa lazima iwasilishwe katika mkutano wa mashauriano kwa Nchi Wanachama 200 ili iweze kupitishwa.
"Kama nakala hii itapitishwa, itakuwa ya" kihistoria kwa ulinzi wa asili WWF. "Rasimu hii ni uboreshaji wa kweli kwenye toleo la awali, ambalo lilichochea hasira. Lugha inayozunguka nishati ya kisukuku imeimarishwa, lakini bado inashindwa kutoa wito wa kuondoka kabisa kutoka kwa makaa ya mawe, mafuta na gesi. Nakal hiyo inatoa wito kwa nchi kufuata sayansi ya tabia nchi ya IPCC na inalenga kupunguza ongezeko la joto hadi 1.5°C, lakini mwongozo huo hauambatani kikamilifu na lengo. "
(Taarifa zaidi zinakujia...)